Zimetajwa sababu za wanandoa kukimbiana harusini

Kila asubuhi Millard Ayo atazisogeza karibu yako habari zote kubwa kutoka kwenye Magazeti mbalimbali ya Tanzania ambapo huwa naziweka kwenye page ya Twitter ya @millardayo na kwenye Youtube ya millardayo bila kusahau millardayo.com.
Moja ya habari iliyoandikwa leo ni hii kutoka gazeti la Jambo leo yenye kichwa cha habari ‘Sababu za wanandoa kukimbiana harusini’.
Baada ya kuwepo kwa mfululizo wa wa matukio ya wapenzi kukimbiana siku ya harusi, gazeti la Jambo leo limezungumza na mtaalamu wa Saikolojia na uhusiano wa chuo kikuu cha Dar es salaam, Dk. Chris Mauki amezitaja sababu za watu wengi kukimbiana siku ya harusi ikiwemo ni pamoja na kutofahamiana vizuri, kuhifadhi vitu mioyoni na wasiwasi juu ya ndoa baina ya wapenzi